Mwanzo    Nyumbani    Links   Kurasa ya kijani    Tafuta  



Larijani: Rekodi ya haki za binadamu ya Iran ni nzuri zaidi Mashariki ya Kati
Namba: 278868 Tarehe: 1390/00/00Rejea: tehranprint

Larijani: Rekodi ya haki za binadamu ya Iran ni nzuri zaidi Mashariki ya Kati

Mkuu wa Baraza la Haki za Binadamu la Iran amesema rekodi ya Tehran ya haki za binadamu ni nzuri zaidi ikilinganishwa na nchi nyingine za Mashariki ya Kati 

 Larijani: Rekodi ya haki za binadamu ya Iran ni nzuri zaidi Mashariki ya Kati
Akihutubia hii leo mjini New York Marekani pambizoni mwa Mkutano wa Kamati ya 3 ya Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa Muhammad Javad Larijani ameongeza kwamba, madai yanayotolewa na Marekani na washirika wake kwamba Iran inavunja haki za binadamu ni sehemu ya siasa za Washington katika eneo hili. Aidha Larijani amesema Marekani haina nia ya kuimarisha demokrasia bali lengo lake ni kufuatilia maslahi yake haramu katika njia ambazo zinakwenda kinyume na demokrasia katika eneo la Mashariki ya Kati. Mkuu wa Baraza la Haki za Binadamu la Iran aidha ameashiria kushiriki Marekani katika vitendo kadhaa vya kigaidi dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na kueleza kwamba, Washington inaunga mkono makundi ya kigaidi kama vile Tondar, Rigi na Mujahedin Khalq na kusema kuwa hiyo ni mifano ya wazi inayoonyesha jinsi Marekani inavyokiuka haki za binadamu. 
 




Barua pepe:
Jina:
Ujumbe:
Enter security code
erfan
ABNA World Service
Englishالعربية
Françaisاردو
Españolفارسی
Русский中文
DeutschTürkçe
Azeri (cyr) Azeri (ltin)
Melayu Indonesia
বাংলা हिन्दी
Swahili Myanmar
BosanskiABP sites
  Habari za Zamani