Rais wa Sudan Kusini ametoa ombi hilo leo alipokutana na kufanya mazungumzo na Rais Mwai Kibaki wa Kenya katika ikulu ya Nairobi. Kwenye mazungumzo hayo Rais Kiir aliishukuru serikali ya Kenya kwa kuendelea kufuatilia kwa karibu mchakato wa amani kati ya Khartoum na Juba na ameitaka Nairobi kuendeleza ufuatiliaji huo katika masuala ambayo bado yanazigonganisha vichwa pande mbili hizo. Rais Mwai Kibaki kwa upande wake amesema Kenya itahakikisha inaendelea kusisitiza utekelezwaji kamili wa makubaliano ya amani ya Naivasha ya mwaka 2005 kati ya Sudan Kusini na Sudan.