Kikundi cha Ikhwanul Muslimina imetoa ujumbe asubuhi ya leo katika mtandao wa Twitter kuwa Dokta Muhammad Mirsiy ndiye Rais wa kwanza wa uchaguzi huru ulofanyika nchi humo.
Kikundi hicho kiliyatangaza hayo baada ya kuhesabiwa kura zote na kupata ushindi mgombea wa chama hicho, na kumtangaza kuwa yeye ndiye Rais wa Misri, ama mpaka hivi sasa tume ya uchaguzi bado haijatoa matokeo ya uchaguzi huo.