| Namba: 331808 | Tarehe: 2012/07/25 - 23:15 | Rejea: ABNA.ir | print |
Ripoti ya shirika la habari la Ahlul Bayt(as)-ABNA- Tovuti ya Al-Wafaq imearifu kuwa; Utawala wa Alikhalifa bado waendelea na opresheni zake za kukandamiza Wananchi wa Bahrain bila kujali fadhila na Baraka za Mwezi Mtukufu wa Ramadhani.
Aidha Tovuti hiyo ilisema: Vikosi vya usalama vya utawala Bahrain bado vya endelea na opresheni zake kupiga waandamanaji katika Mwezi Mtukufu wa Ramadhani bila kujali fadhila na Baraka za Mwezi wa Ramadhani, siku Tatu zilizopita watu Nane walitiwa mbaroni na Tisa kujeruhiwa, unyama na opresheni hizo zaendelea katika sehemu 31 za Nchi hiyo ili kuzuiya maandamano.

Polisi ya Bahrain yatumia silaha zinazopigwa marufuku na Umoja wa Kimataifa kama Gesi ya Sumu, Risasi za Plastiki na Mabomu ya Sauti.
Pia Polisi hao watukana watu na kuvuliwa heshima Wanawake, na kila atakae kamatwa hupigwa vibaya nusu ya kuuliwa.

Aidha Kijiji cha Al-Dir waliandamana kwa kupinga vitendo vichafu vya Polisi kushambulia watu walokua wakifuturu katika Kijiji cha Al-kurah.
Aidha Vijiji vya Al-sitra, An-Nwidarat, Wa`dian, Akr, Kha`arijiah, Bani Jamrah, Jadd Aliy, Deraz, Abul Aish, Diir, Sanad, Muswala na Diah vilivamiwa na kupigwa watu vibaya na walokuwa wengi walipelekwa Hospitali.






