Mwanzo    Nyumbani    Links   Kurasa ya kijani    Tafuta  



Kikao cha wawakilishi wa taasisi za Qur'ani chafanyika Madrid
Namba: 280538 Tarehe: 1390/00/00Rejea: iqnaprint

Kikao cha wawakilishi wa taasisi za Qur'ani chafanyika Madrid

Kikao cha wawakilishi wa taasisi za Qur'ani Tukufu kilifanyika Alkhamisi iliyopita huko Madrid mji mkuu wa Hispania. 

 Kikao cha wawakilishi wa taasisi za Qur
Kwa mijibu wa tovuti ya Shirika la Elimu, Sayansi na Utamaduni la Jumuiya ya Ushirikiano wa Kiislamu ISESCO, lengo la maudhui zilizojadiliwa katika kikao hicho, na ambazo ziliandaliwa kwa ushirikiano wa ISESCO na Jumuiya ya Kimataifa ya Hifdhi ya Qur'ani pamoja na Jumuiya ya Qur'ani ya Hispania, lilikuwa ni kuimarisha ratiba za masomo ya Qur'ani barani Ulaya.
Washiriki wa kikao hicho wamesisitiza juu ya umuhimu wa kuimarishwa mipango yamasomo ya Qur'ani barani Ulaya. Wametaka pia kuasisiwa madrasa, shule na vituo vya masomo ya Kiislamu barani humo.
Vilevile washiriki wameelezea azma yao ya kuunga mkono juhudi zinazofanyika kwa lengo la kuasisiwa taasisi muhimu ya Kiislamu pamoja na uimarishwaji wa masomo ya Qur'ani barani Ulaya.
 




Barua pepe:
Jina:
Ujumbe:
Enter security code
erfan
ABNA World Service
Englishالعربية
Françaisاردو
Españolفارسی
Русский中文
DeutschTürkçe
Azeri (cyr) Azeri (ltin)
Melayu Indonesia
বাংলা हिन्दी
Swahili Myanmar
BosanskiABP sites
  Habari za Zamani