Ripoti ya shirika la habari la Ahlul Bayt(as)-ABNA-Ahmad Abdunnabii mwenye umri wa miaka 31 aliaga Dunia kwa athari ya Gesi ya simu inayotumiwa na vikosi vya usalama vya Alikhalifa katika makazi ya watu Nchini humo, pia walipelekwa wakazi wengine Ospitslini kwa athari ya Gesi hiyo.
Wananchi wa Bahrain jana walimbeba shahidi huyo”Abduh Ali Abdul Husein” na kulaani vikali kitendo cha utawala dhalimu wa Alikhalifa Bahrain kwa kuuwa watu kwa kutumia Gesi ya sumu Nchini humo.
Katika mazishi hayo walishiriki mamia ya Wananchi kuutaka utawala Bahrain kujitoa katika mamlaka ya nchi.
Unyama unaofanyika Nchini Bahrain umekaza kimya Dunia nzima hasa wanaojiita kuwa wao ni watetezi wa haki za binadamu mfano wa Marekani, ipo wazi Marekani ipo tayari kuhami maovu ili kulinda maslahi yake, kama inavyounga mkono Saudia Arabia kwa kukandamiza Wananchi wake hasa kwa kile kinachofanywa na utawala wa Bahrain ili kulinda maslahi yake.
Kuuawa Ahmad Abdul Nnabii imeongeza idadi ya mashihid Bahrain kufikia 80.