| Namba: 313849 | Tarehe: 2012/05/09 - 09:58 | Rejea: | print |
Viongozi wa vyama vya New Democracy na kile cha Pasok hapo jana walishindwa kuafikiana kuhusu uundwaji wa serikali mpya ya umoja wa kitaifa baada ya kutokea kutoelewana kuhusu muundo wa serikali
Wananchi wa Ugiriki waliopiga kura siku ya Jumapili waliamua kupigia kura vyama vingine vya upinzani ambavyo vilikuwa mstari wa mbele kupinga hatua ya serikali ya kubana matumizi hatua iliyoelezwa ni kuchukizwa na iliyokuwa serikali ya umoja wa kitaifa iliyopitisha hatua za ubanaji wa matumizi.
Nchi hiyo iliamua kukubali mpango wa kubana matumizi kwa lengo la kupatiwa msaada wa fedha wa zaidi ya Euro bilioni 240, fedha ambazo zingetumika kunusuru uchumi wa taifa hilo.
Hapo jana kansela wa Ujerumani Angela Markel amenukuliwa akiwataka viongozi na wananchi wa Ugiriki kukubalina na masharti ya ubanaji wa matumizi ambayo ni muhimu kwaajili ya kuinusuru nchi hiyo.
Tayari hofu imeanza kutanda kwenye baadhi ya nchi wananchama wa Umoja huo ambao wanaona endapo Ugiriki ikishindwa kuwa na serikali itakayokubali kubana matumizi basi hali ya uchumi kwenye mataifa mengine ya Ulaya itaendelea kuwa mbaya zaidi.
Nchi ya Ugiriki ililazimika kupunguza wafanyakazi wa umma na kupitisha bajeti ya ubanaji wa matumizi ya Serikali.