Hissene Habre, anashitakiwa kwa makosa ya kukiuka haki za binadamu wakati wa utawala wake mnano miaka ya 1982 - 1990.
Kesi hii dhidi ya Hissene Hebre ilifunguliwa na raia wa Ubeligiji mwenye asili ya Chad kwa madai kuwa wakati wa utawala wa Hissene Hebre watu wapatao 40,000 waliteswa na hata wengine kupoteza maisha.
Hissene Hebre yupo ukimbizini nchi Senegal ambako alikimbilia baada ya utawala wake kuondolewa.