| Namba: 333632 | Tarehe: 2012/08/01 - 17:35 | Rejea: ABNA.ir | print |
Bashar Al-Asad awasifu wanajeshi wake |
Katika tamko alilolitoa kwenye maadhimisho ya siku ya jeshi nchini Syria,
rais Assad alisema kwamba hatima ya raia wa nchi hiyo, pamoja na taifa, kwa
ujumla, inategemea vita vinavyoendelea kati ya waasi na wanajeshi wa Syria.
Tangu kuuwawa kwa maafisa wakuu wa nne wa jeshi lake wiki mbili zilizopita,
Assad hajazungumza tena hadharani. Assad aliwasifu wanajeshi wake na kusema
kwamba ana imani kubwa na kile wanachokifanya.