Mwanzo    Nyumbani    Links   Kurasa ya kijani    Tafuta  



Serikali ya Ugiriki wakutana kujadili swala la kuomba mkopo kutoka IMF
Namba: 333680 Tarehe: 2012/08/01 - 22:46Rejea: ABNA.irprint

Serikali ya Ugiriki wakutana kujadili swala la kuomba mkopo kutoka IMF

Viongozi wa Serikali ya Umoja ya Ugiriki wanakutana kwa mara ya tatu hii leo kwa ajili ya kujadili utekelezaji wao katika kuhakikisha wanapata mkopo wa euro bilioni kumi na moja nukta tano kutoka Umoja wa Ulaya na Shirika la Fedha Duniani IMF. 

 Serikali ya Ugiriki wakutana kujadili swala la kuomba mkopo kutoka IMF

Viongozi hawa wanakutana ili kuhakikisha mkakati wao wa kupata mkopo kutoka EU na IMF unafanikiwa ili kujiepusha na hali mbaya ya kiuchumi ambayo wanakabiliwa nayo kwa sasa.

Naibu waziri wa Fedha Christos Staikouras amesema wameshapiga hatua nzuri na anamini Viongozi hao watakubaliana katika utekelezaji wa kile ambacho wamekipanga ili kufanikisha malengo yao.

Miongoni mwa vitu ambavyo Viongozi hao wanastahili kukubaliana ni pamoja na kubana matumizi ili kutekeleza moja ya sharti la Umoja wa Ulaya EU ili waweze kupata mkopo huo na kupiga hatua.

Mkutano huu unakuja siku kadhaa baada ya Rais wa Tume ya Umoja wa Ulaya EU kutembelea Athens na kuitaka serikali kuhakikisha inaonesha njia ya kukabiliana na hali ngumu na kudorora kwa uchumi.

 




Barua pepe:
Jina:
Ujumbe:
Enter security code
erfan
ABNA World Service
Englishالعربية
Françaisاردو
Españolفارسی
Русский中文
DeutschTürkçe
Azeri (cyr) Azeri (ltin)
Melayu Indonesia
বাংলা हिन्दी
Swahili Myanmar
BosanskiABP sites
  Habari za Zamani